π Mahitaji:
π₯£ Unga wa ngano – nusu kilo
π§΄ Hamira – kijiko 1 kikubwa
π₯ Maziwa – nusu lita (yawe ya uvuguvugu)
π¬ Sukari – vijiko 3 vya chakula (zaidi kwa kujazia)
π° Mdalasini ya unga (cinnamon powder) – kiasi cha kupaka
π§ Chumvi – robo kijiko cha chai
π§ Margarine – vijiko 3 vya chakula (zaidi kwa kupaka juu)
π©π½π³ Maandalizi:
1. Tayarisha Hamira:
π₯ Changanya maziwa kidogo ya uvuguvugu na hamira kwenye kikombe. Acha ifure kwa dakika 5.
2. Changanya Unga:
Weka unga kwenye bakuli kubwa. Ongeza sukari π§, chumvi π§, na margarine vijiko 3. Changanya vizuri kwa mkono au kijiko.
3. Ongeza Hamira:
Mimina mchanganyiko wa hamira kwenye unga. Endelea kuchanganya huku ukiongeza maziwa ya uvuguvugu taratibu.
4. Kanda Mchanganyiko:
Kanda unga mpaka uwe laini kiasi – usiwe mgumu sana wala mlaini kupita kiasi.
π Acha uumuke (ukae hadi uvimbe mara mbili ya kiasi cha awali).
5. Tengeneza Rolls:
Kata madonge makubwa, kisha sukuma kama chapati – lakini iwe pana na sio nyembamba sana.
6. Paka na Roll:
Paka margarine juu ya donge lililosukumwa π§, nyunyiza sukari π¬ na mdalasini ya unga π°.
Kisha roll (kunja kama chapati) mpaka mwisho.
7. Kata na Panga:
Tumia kisu kukata vipande, kisha panga kwenye trey au sufuria kwa kuoka.
πΆ Topping:
Baada ya rolls kuiva, mimina maziwa ya sona π₯ au homemade condensed milk juu yake kwa ladha ya kipekee. π
Tip: Unaweza kuzila zikiwa moto au baridi – zote ladha yake ni ya kupendeza sana! π§❤️
Maoni