Mahitaji
Mayai ya kuchemsha – 4 hadi 6 (kisha uyakatwe nusu au uyachemshe tu)
Kitunguu maji – 2 vikubwa (katakata vizuri)
Nyanya – 2 vikubwa (menya na saga/blend au katakata)
Kitunguu saumu na tangawizi – 1 kijiko cha chakula (iloweke na saga kwa pamoja)
Pilipili hoho – nusu (hiari, katakata)
Mafuta – 3 vijiko vya chakula
Binzari ya manjano (turmeric) – nusu kijiko cha chai
Garam masala – nusu kijiko cha chai
Poda ya coriander – 1 kijiko cha chai
Pilipili ya unga – kiasi (kulingana na ladha)
Majani ya giligilani (coriander leaves) – kwa kupambia
Chumvi – kiasi
Maji – kikombe 1 hadi 1½
Namna ya Kupika.π³
π³ Chemsha mayai kwa dakika 8–10 hadi yawe magumu.
π³Yavue maganda, halafu unaweza kuyachoma kidogo kwenye mafuta (hiari) ili yawe na ladha zaidi na yasivunjike kirahisi.
π³Weka mafuta kwenye sufuria moto wa wastani.
π³ Ongeza vitunguu maji ulivyokatakata, kaanga hadi viwe vya hudhurungi (golden brown).
π³Ongeza mchanganyiko wa tangawizi na kitunguu saumu, pika dakika 1–2 hadi harufu nzuri itoke.
π³ Ongeza nyanya zilizosagwa au kukatakata. Pika hadi ziyeyuke na ziunde mchuzi mzito.
π³Weka viungo: binzari ya manjano, coriander powder, pilipili ya unga, na chumvi. Koroga vizuri.
π³Ongeza maji kiasi, funika na uache ichemke kwa dakika 5–7.
π³ Kata mayai nusu (hiari) au uweke mazima.
π³ Yaweke kwa upole ndani ya mchuzi. Koroga kwa uangalifu usiyavunje.
π³ Punguza moto na acha ichemke kwa dakika nyingine 5 ili ladha iingie ndani ya mayai.
π³ Nyunyiza garam masala na majani ya giligilani.
π³Funika kwa dakika 1, kisha ipua.
Maoni