Mahitaji
Nyama ya kusaga (kiasi unachotaka)
Viungo vya nyama ya kusaga:
Kitunguu saumu (thomu)
Tangawizi
Pilipili manga
Mdalasini ya unga
Karafuu ya unga
Chumvi
Maganda ya limao au limao
Pilipili ya kusaga (optional)
Mayai 3
Karoti 1 (iliyokatwakatwa au kupgrated)
Kitunguu maji 1-2
Pilipili hoho (pili pili boga)
Curry powder
Piki m powder (au garam masala)
Pilipili ya kusaga (ya kuwasha)
Baking paper
Mafuta ya kukaanga
Maelekezo:
1. Pika Nyama ya Kusaga
Weka nyama ya kusaga kwenye sufuria.
Ongeza viungo vyote vya kusaga nyama (kitunguu saumu, tangawizi, pilipili manga, mdalasini, karafuu, chumvi, nk).
Usiongeze maji. Pika hadi nyama iive na ikauke maji yake ya asili.
2. Andaa Mchanganyiko
Katika blender, weka:
Mayai 3
Nyama uliyopika
Karoti
Kitunguu maji
Pilipili hoho
Saga hadi mchanganyiko uwe laini kabisa.
3. Ongeza Viungo vya Ladha
Mimina mchanganyiko kwenye bakuli.
Ongeza curry powder, piki m powder, na pilipili ya kusaga (ya kuwasha).
Koroga vizuri hadi kila kitu kichanganyike sawasawa.
4. Oka Mchanganyiko
Washa oveni yako kwa nyuzijoto 180°C.
Tandika baking paper kwenye treya ya kuokea.
Mimina mchanganyiko juu ya baking paper kwa usawa.
Oka hadi mchanganyiko uwe umeiva na umekauka vizuri (kama mkate wa nyama).
5. Kata Triangle
Baada ya kuiva, toa kutoka kwenye oven.
Acha ipoe kidogo kisha kata umbo la pembetatu (triangle).
6. Kaanga Triangle
Piga yai kwenye bakuli.
Chovya kila triangle kwenye mayai yaliyopigwa.
Kaanga kwenye mafuta ya moto hadi ziwe golden brown.
Tayari Kula!
Unaweza kula triangle hizi na chai, juisi au hata kachumbari kama kando
Maoni