πŸ₯₯ NJUGU MAWE ZA TUI LA NAZI πŸ₯œ

πŸ₯₯ NJUGU MAWE ZA TUI LA NAZI πŸ₯œ



πŸ“Œ MAHITAJI

✅ 250g (robo kilo) njugu mawe 🌰
✅ 1 nazi πŸ₯₯
✅ 10 punje za hiliki 🌿
✅ 5 vijiko vya chakula sukari 🍚
✅ 1 kijiko cha chakula custard powder ✨
✅ 1 kijiko cha chai arki (vanilla) 🌼
✅ Chumvi kidogo πŸ§‚




πŸ“ MAANDALIZI

1️⃣ Chagua njugu mawe zako – Ondoa mawe na uchafu wote.
2️⃣ Osha vizuri – Zisuuze kwa maji safi kisha weka kwenye chombo.
3️⃣ Tayarisha tui – Kata nazi yako na kamua tui:

Tui zito (kikombe kidogo cha chai)

Tui jepesi (kibakuli kimoja)
4️⃣ Menya na twanga hiliki – Changanya na sukari kidogo ili ipate harufu nzuri.
5️⃣ Changanya custard – Katika tui zito, changanya custard powder na weka pembeni.





πŸ‘¨‍🍳 JINSI YA KUPIKA

1️⃣ Chemsha njugu – Weka njugu kwenye sufuria na maji kiasi. Pika kwa moto mdogo huku ukiweka maji kidogo kidogo hadi ziive vizuri.
2️⃣ Ongeza tui jepesi – Mimina tui jepesi, hiliki iliyosagwa, sukari, na chumvi. Acha ichemke hadi tui lipungue.
3️⃣ Mimina tui zito na arki – Ongeza tui zito lililochanganywa na custard pamoja na arki ya vanilla.
4️⃣ Acha ichemke kidogo – Ikiwa nzito na harufu nzuri imeenea, epua.
5️⃣ Tayari kwa kula – Furahia njugu zako na chapati, mkate wa ufuta, boflo, au mkate wowote.




⚠️ ANGALIZO

πŸ”Ή Usiweke maji mengi wakati wa kuchemsha njugu ili zisiharibike na kubanduka maganda.
πŸ”Ή Usitumie custard nyingi – Itafanya mchanganyiko uwe mzito kupita kiasi na kupoteza ladha yake.
πŸ”Ή Usimimine tui jingi jepesi – Njugu zitakuwa nyepesi badala ya kuwa nzito na tamu.
πŸ”Ή Usikoroge kwa mwiko – Badala yake, itikise sufuria kwa kushikilia kwa banio la ugali au kitambaa safi cha jikoni.

πŸ₯œ Furahia Njugu Mawe zako! πŸ˜‹


Maoni