π₯₯ NJUGU MAWE ZA TUI LA NAZI π₯
π₯₯ NJUGU MAWE ZA TUI LA NAZI π₯
π MAHITAJI
β
250g (robo kilo) njugu mawe π°
β
1 nazi π₯₯
β
10 punje za hiliki πΏ
β
5 vijiko vya chakula sukari π
β
1 kijiko cha chakula custard powder β¨
β
1 kijiko cha chai arki (vanilla) πΌ
β
Chumvi kidogo π§
π MAANDALIZI
1οΈβ£ Chagua njugu mawe zako β Ondoa mawe na uchafu wote.
2οΈβ£ Osha vizuri β Zisuuze kwa maji safi kisha weka kwenye chombo.
3οΈβ£ Tayarisha tui β Kata nazi yako na kamua tui:
Tui zito (kikombe kidogo cha chai)
Tui jepesi (kibakuli kimoja)
4οΈβ£ Menya na twanga hiliki β Changanya na sukari kidogo ili ipate harufu nzuri.
5οΈβ£ Changanya custard β Katika tui zito, changanya custard powder na weka pembeni.
π¨βπ³ JINSI YA KUPIKA
1οΈβ£ Chemsha njugu β Weka njugu kwenye sufuria na maji kiasi. Pika kwa moto mdogo huku ukiweka maji kidogo kidogo hadi ziive vizuri.
2οΈβ£ Ongeza tui jepesi β Mimina tui jepesi, hiliki iliyosagwa, sukari, na chumvi. Acha ichemke hadi tui lipungue.
3οΈβ£ Mimina tui zito na arki β Ongeza tui zito lililochanganywa na custard pamoja na arki ya vanilla.
4οΈβ£ Acha ichemke kidogo β Ikiwa nzito na harufu nzuri imeenea, epua.
5οΈβ£ Tayari kwa kula β Furahia njugu zako na chapati, mkate wa ufuta, boflo, au mkate wowote.
β οΈ ANGALIZO
πΉ Usiweke maji mengi wakati wa kuchemsha njugu ili zisiharibike na kubanduka maganda.
πΉ Usitumie custard nyingi β Itafanya mchanganyiko uwe mzito kupita kiasi na kupoteza ladha yake.
πΉ Usimimine tui jingi jepesi β Njugu zitakuwa nyepesi badala ya kuwa nzito na tamu.
πΉ Usikoroge kwa mwiko β Badala yake, itikise sufuria kwa kushikilia kwa banio la ugali au kitambaa safi cha jikoni.
π₯ Furahia Njugu Mawe zako! π
Maoni