JINSI YA KUPIKA KATLESI ZA NYAMA

Jinsi ya kupika KATLESI za Nyama




mahitaji
-viazi mbatata - Β½
-Nyama ya kusaga robo
-Mayai 3
-Vitunguu maji Vikubwa 2 
-pilipili hoho 1
-karoti 1
-Ndimu / limau 
-Pilipili manga - kijiko cha chai Β½
-Tangawizi mbichi 
-Kitunguu thomu 
-Bizari ya mchuzi kijiko cha chai 1 
-chumvi kiasi
-Chenga za mkate (Bread crumbs) Weka katika sahani -kikombe 1cha mafuta ya kupikia


Namna ya kupika:
-Menya viazi vikate na uchemshe vikiwa vinakaribia kuiva weka binzari ya manjano, ndimu na chumvi, vitunguu maji, hoho na karoti(iliyokwanguliwa) kisha utaviponda kwa pamoja mpka viwe kama ugali.

-Chemsha Nyama kwa tangawizi na kitunguu thomu, pilipilimanga mpaka ikauke. 

- Sasa changanya vizuri na viazi ulivyoviponda ponda na nyama uliyoitia viungo, changanya vizuri mpaka viazi vichanganyike vizuri na nyama.

-Sasa fanya madonge na uviringe kama shepu ya yai au duara kawaida.

-Sasa vunja yale mayai kisha uyakoroge kwenye kibakuli pembeni, baada ya chukua vile viazi vyenye shepu ya duara uvigaragaze kwenye chenga za mkate, vyote viwe vimepakwa chenga za mkate; kisha utachovya kwenye ute wa yai na kuzichoma kwenye mafuta mpaka ziwe na rangi ya dhahabu.
baada ya hapo tayari kuliwa.

NB:- unaweza kutumia nyama ya kuku, au samaki bila kusahau kutoa miba.

-kama hauna chenga za mkate unaweza kutumia unga wa ngano uliochanganywa na sembe kidogo.

-Epuka kugeuza geuza ili zisije zikavurugika kwenye mafuta, na mafuta yawe yamepata moto kiasi kwani zikikaa sana jikoni pia zinaweza kuvurugika.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

JINSI YA KUPIKA MIKATE YA CHILA (VIBIBI)

🌿πŸ₯©πŸŒNDIZI ZA NYAMA

VILEJA VYA JICHO LA NGAMIA

πŸ₯©πŸ₯—πŸ›BIRIANI YA NYAMA YA NG'OMBE

πŸ—πŸ₯˜πŸ²PILAU YA KUKU

JINSI YA KUPIKA NJEGERE ZA NAZI 🍲

πŸͺ🍯VILEJA VYA CARAMEL

JINSI YA KUPIKA VITUMBUA

🌼🌺VILEJA VYA JAM