🌿πŸ₯©πŸŒNDIZI ZA NYAMA

 

NAMNA YA KUPIKA NDIZI ZA NYAMA



MAHITAJI

🍌 Ndizi mbichi - 10-12
πŸ₯© Nyama ng’ombe - 1 kilo moja
πŸ§… Kitunguu maji - 2
πŸ… Nyanya/tungule - 2
πŸ§„ Kitunguu saumu (thomu/galic) - 7
πŸ§‘‍🍳 Tangawizi mbichi - 1 kipande
πŸ‹ Ndimu - 2 kamua
πŸ§‚ Chumvi - kiasi
πŸ›’ Mafuta - 3 vijiko vya supu
πŸ₯₯ Tui la nazi - 3 vikombe


Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

  1. πŸ§„ Saga kitunguu thomu na tangawizi mbichi.
  2. πŸ₯© Weka nyama katika sufuria, tia kijiko kimoja cha kitunguu thomu na tangawizi, chumvi, na ndimu, kisha chemsha hadi iive.
  3. 🍌 Menya ndizi na ukatekate.
  4. πŸ›’ Weka mafuta katika sufuria, tia kitunguu maji kilokatwakatwa, ukaange kidogo tu, kisha tia nyanya/tungule uendelee kukaanga.
  5. πŸ§„ Tia tangawizi na thomu iliyobakia.
  6. 🍌 Tia ndizi, kaanga kidogo kisha tia supu ya nyama na nyama yake.
  7. 🍽 Ziache ndizi ziive, zikiwa tayari tia tui la nazi.


Maoni