NAMNA YA KUPIKA NDIZI ZA NYAMA
MAHITAJI
π Ndizi mbichi - 10-12
π₯© Nyama ng’ombe - 1 kilo moja
π§
Kitunguu maji - 2
π
Nyanya/tungule - 2
π§ Kitunguu saumu (thomu/galic) - 7
π§π³ Tangawizi mbichi - 1 kipande
π Ndimu - 2 kamua
π§ Chumvi - kiasi
π’ Mafuta - 3 vijiko vya supu
π₯₯ Tui la nazi - 3 vikombe
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
- π§ Saga kitunguu thomu na tangawizi mbichi.
- π₯© Weka nyama katika sufuria, tia kijiko kimoja cha kitunguu thomu na tangawizi, chumvi, na ndimu, kisha chemsha hadi iive.
- π Menya ndizi na ukatekate.
- π’ Weka mafuta katika sufuria, tia kitunguu maji kilokatwakatwa, ukaange kidogo tu, kisha tia nyanya/tungule uendelee kukaanga.
- π§ Tia tangawizi na thomu iliyobakia.
- π Tia ndizi, kaanga kidogo kisha tia supu ya nyama na nyama yake.
- π½ Ziache ndizi ziive, zikiwa tayari tia tui la nazi.
Maoni