JINSI YA KUPIKA CAKE ILIYOCHAMBUKA NA VIPIMO VYAKE

JINSI YA KUPIKA CAKE ILIYOCHAMBUKA NA VIPIMO VYAKE



Ukitaka kupika cake iliyochambuka vizuri 🍰:

1. Baking powder ichanganye na unga kisha chekecha unga mara mbili au zaidi ili ichanganyanyike vizuri 🧁.


2. Saga sukari na blueband/kimbo/samli mpaka sukari iwe laini kusiwe na machenga chenga na iwe nyeupe na ivimbe ndipo uanze kueka mayai 🧈🍯.


3. Wakati wa KUEKA mayai, weka moja uchanganye kisha jingine hivyo hivyo mpaka yaishe, usieke yote kwa pamoja 🥚.


4. Weka maziwa/maji ya limao au maji ya chungwa katika cake yako (hii inasaidia cake ichambuke sana ndani) 🥛🍋🍊.


5. Wakati wa KUEKA unga, punguza speed ya mashine, ikiwezekana tumia mwiko badala ya mashine kuchanganya unga… na usikoroge kwa muda mrefu, ukishanganyika basi inatosha 🥄.


6. Moto wa kuoka cake usiwe mwingi, cake haitaki moto mwingi, inahitaji joto (mvuke) wa wastani 🌡️.



VIPIMO VYA CAKE

Fata vipimo vya cake hivi👇
Keki

Mayai 12 🥚

Sukari 1/2 🍬

Siagi 1/2 🧈

Unga 1/2 na viganja 2 🍚

Baking powder 2tsp 🧁


Keki

Mayai 10 🥚

Sukari 1/2 🍬

Siagi 1/2 🧈

Unga 1/2 na kiganja 1 🍚

Baking powder 2tsp 🧁


Keki

Mayai 8 🥚

Sukari 1/2 punguza kidogo 🍬

Siagi 1/2 🧈

Unga 1/2 🍚

Baking powder 2tsp 🧁


Keki

Mayai 6 🥚

Sukari 1/4 🍬

Siagi 1/4 🧈

Unga 1/4 🍚

Baking powder 1 tsp 🧁

Maoni