πŸ₯—πŸ—πŸ₯™WALI WA TAMBI NA SAUCE YAKE YA KUKU

 JINSI YA KUPIKA WALI WA TAMBI NA MCHUZI WAKE WA KUKU

Vipimo Vya Wali 🍚                  

  • Mchele - 3 vikombe
  • Tambi - 2 vikombe                                                                                      
  • Mafuta - ¼ kikombe
  • Chumvi - Kiasi


Vipimo Vya Kuku πŸ—

  • Kuku kidari (boneless) aliyekatwa katwa vipande - 1 kilo
  • Kitunguu maji kilichokatwa katwa - 2
  • Kitunguu saumu (thomu/galic) na tangawizi iliyosagwa - 1 kijiko cha supu
  • Pilipili mbichi iliyosagwa - 1 kijiko cha chai
  • Chumvi - Kiasi
  • Paprika - 1 kijiko cha supu
  • Masala ya kuku (tanduri au yoyote) - 1 kijiko cha supu
  • Ndimu - 2 vijiko vya supu
  • Mtindi (yoghurt) au malai (cream) - 1 kikombe
  • Mafuta - ¼ kikombe
  • Majani ya kotmiri (coriander) - ½ kikombe



Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Wali 🍚

  1. Osha mchele kisha uroweke.
  2. πŸ›’️ Tia mafuta katika sufuria, kisha kaanga tambi zilizokatwakatwa hadi zibadilike rangi kuwa nyekundu.
  3. Tia mchele na endelea kukaanga kwa muda mfupi.
  4. Tia maji kiasi cha wali kupikika, kama unavyopika pilau (maji yanategemea aina ya mchele).
  5. πŸ”₯ Funika na pika katika moto mdogo mdogo hadi wali uive.
  6. Epua ukiwa tayari.

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Kuku πŸ—

  1. Katika bakuli, changanya vitu vyote isipokuwa mtindi na kitunguu.
  2. πŸ›’️ Tia mafuta katika karai, kisha kaanga kitunguu kwa muda mfupi tu (hakikisha hakigeuki rangi).
  3. Tia kuku pamoja na masala yake, kisha endelea kukaanga kwa muda.
  4. πŸ₯› Tia mtindi au malai, kisha funika na pika hadi kuku aive vizuri.
  5. 🌿 Nyunyuzia kotmiri iliyokatwakatwa juu ikiwa tayari.
  6. Tumikia na wali wa tambi kwa ladha ya kipekee! πŸ˜‹

Maoni