JINSI YA KUPIKA VILEJA VYA MCHELE
JINSI YA KUPIKA VILEJA VYA MCHELE
MAHITAJI NA VIPIMO
- 🍚 Unga wa mchele - kilo 1
- 🧈 Samli ya Aseel - nusu (1/2)
- 🍬 Sukari - nusu (1/2)
- 🍶 Arki (vanilla flavour) - kijiko 1 cha chai
- 🥄 Baking powder - 1 kijiko cha chai
- 🥚 Mayai - 3
- 💧 Maji - 1/2 kikombe cha chai
NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA
1️⃣ Saga sukari na samli ya Aseel iwe laini kiasi.
2️⃣ Changanya unga wa mchele, baking powder, na sukari.
3️⃣ Kisha uchanganye pamoja na arki.
4️⃣ Ongeza mayai yaliopigwa na endelea kuchanganya mpaka unga umeanza kuchanganyika vizuri.
5️⃣ Ongeza maji kama nusu kikombe tu ili uchanganyike vizuri.
6️⃣ Kata kwa design unayotaka, visiwe vinene. Kisha weka kwenye mashine yake ya mkono na ukipenda utaweka kidoto kwa kutumia zaafarani katikati ya kileja.
7️⃣ Choma kwa moto wa baina ya 200°F na 250°F kwa dakika 20 mpaka 30. Visiwe vyekundu, toa na tayari kwa kuliwa.
😋 Furahia vileja vyako!
Maoni