🍮 HALUWA(HALWA)

 🍮 JINSI YA KUPIKA HALUWA(HALWA)








MAHITAJI

💧 Vikombe 3 vya maji

🍬 Vikombe 4 vya sukari ya brown

🌼 Bana kidogo ya zafarani iliyochanganywa na vijiko 2 vya maji ya waridi (rose water)

🎨 Bana kidogo ya rangi ya machungwa na nyekundu

🔥 Maji yanapokaribia kuchemka, ongeza:

🥄 Kijiko 1 cha chai cha nutmeg ya unga

🥄 Kijiko 1 na nusu cha chai cha hiliki ya unga

🥣 Vikombe 2 vya unga wa tapioca/cornflour 


kwa kuchanganyia unga

💧 Kikombe 1 cha maji



NAMNA YA KUPIKA HALUA

⿡ Roweka majani ya chai vikombe 2 vya maji ya moto upate rangi iliyokoza.

⿢ Chuja kwenye sufuria kubwa, mimina maji lita tatu na nusu au birika ya umeme mawili ya maji.

⿣ Kwenye hayo maji tia sukari, iliki, maji ya majani ya chai, zafarani na arki. Wacha mpaka ichemke.

⿤ Wakati sufuria ipo jikoni, chukua kibakuli, utie unga wa cornflour na uchanganye na vikombe viwili vya maji ya kawaida.

⿥ Mchanganyiko ukishaanza kuchemka, mimina ule unga uliouchanganya na maji. Koroga bila kuachia mkono kwa kutumia mwiko mrefu.

⿦ Ukiona mchanganyiko umeshashikana sawa sawa, mimina samli vikombe viwili.

⿧ Endelea kukoroga bila kuachia. Mchanganyiko ukiwa mzito, ongeza samli na endelea kukoroga.

⿨ Muda wote koroga kwa mzunguko wa kuelekea upande mmoja tu (clockwise au anticlockwise).

⿩ Koroga kwa masaa mawili hadi mafuta yajitenge na halua, na mchanganyiko uanze kuruka ruka.

⿢ Ili kujua kama halua imeiva, chota kwenye kijiko kidogo na uiache ipoe. Ikiwa ngumu baada ya kupoa, halua iko tayari. Ikiwa laini sana, endelea kupika huku unaendelea kukoroga.

⿡ Ikiwa tayari, tenganisha mafuta yote na halua.

⿡ Mimina halua kwenye trays au vibakuli vya kufunika na upambe kwa lozi zilizokatwa katwa.





Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

JINSI YA KUPIKA MIKATE YA CHILA (VIBIBI)

🌿🥩🍌NDIZI ZA NYAMA

VILEJA VYA JICHO LA NGAMIA

🥩🥗🍛BIRIANI YA NYAMA YA NG'OMBE

🍗🥘🍲PILAU YA KUKU

JINSI YA KUPIKA NJEGERE ZA NAZI 🍲

🍪🍯VILEJA VYA CARAMEL

JINSI YA KUPIKA VITUMBUA

🌼🌺VILEJA VYA JAM