JINSI YA KUPIKA BEEF TAMARIND

JINSI YA KUPIKA BEEF TAMARIND



MAHITAJI 

  • Nyama ya ng'ombe – 1 kg (ikatwa vipande vidogo)
  • Chumvi – Kiasi
  • Ukwaju – Kiasi
  • Beef masala – Kiasi
  • Vitunguu thoum – Kiasi
  • Pilipili mtama – Kiasi
  • Tangawizi – Kiasi
  • Mafuta ya kupikia – Kidogo
  • Carrot – 1 (kikata vipande vidogo)
  • Hoho – 1 (kikata vipande vidogo)
  • Vitunguu maji – 2 (vikatwe)
  • Pilipili – 2 (zikatwe)


MAELEKEZO:

1️⃣ Andaa nyama ya ng'ombe - Kataa nyama kwa vipande vidogo, osha vizuri na uchuje maji.
2️⃣ Changanya viungo - Tia chumvi, ukwaju, beef masala, vitunguu thoum, pilipili mtama, tangawizi, na mafuta kidogo ya kupikia kwenye nyama.
3️⃣ Weka kwenye fridge - Changanya viungo vyote vizuri na weka nyama kwenye fridge kwa masaa 6 ili viungo vimeng'ane.
4️⃣ Chemsha nyama - Toa nyama kutoka kwenye fridge, weka jikoni na iache icheke mpaka inakaribia kujikaanga yenyewe.
5️⃣ Tia mboga - Ongeza karoti, hoho, vitunguu maji viwili, na pilipili mbili. Acha vichemke kiasi mpaka vikajikaange vyenyewe.
6️⃣ Funika na foil - Ipua nyama, weka mafuta kidogo kwenye kikaango kisha funika kwa foil. Weka kikaango kwenye moto ili moshi usitoke nje.
7️⃣ Pika mpaka iive - Acha nyama ikae kwa muda ili viungo vyote vimeng'ane, kisha funua foil na iache ikae kidogo.
8️⃣ Tayari kwa kuliwa - Nyama inakuwa na ladha ya kimishkaki, sasa iko tayari kuliwa!

Ladha ya Beef Tamarind itakuwa tamu na ya kuvutia, kama mishkaki!


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

JINSI YA KUPIKA MIKATE YA CHILA (VIBIBI)

🌿🥩🍌NDIZI ZA NYAMA

VILEJA VYA JICHO LA NGAMIA

🥩🥗🍛BIRIANI YA NYAMA YA NG'OMBE

🍗🥘🍲PILAU YA KUKU

JINSI YA KUPIKA NJEGERE ZA NAZI 🍲

🍪🍯VILEJA VYA CARAMEL

JINSI YA KUPIKA VITUMBUA

🌼🌺VILEJA VYA JAM