🥩🥗🍛BIRIANI YA NYAMA YA NG'OMBE
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
NAMNA YA KUPIKA BIRIANI YA NYAMA YA NG'OMBE
VIPIMO VYA MASALA
- Nyama vipande: 3 LB 🥩
- Mtindi: ½ kopo 🥄
- Kitunguu (thomu/galic): 1½ kijiko cha supu 🧄
- Tangawizi: 1½ kijiko cha supu 🌿
- Nyanya: 2 🍅
- Pilipili mbichi: kiasi 🌶️
- Nyanya kopo: 4 vijiko vya supu 🍅
- Vidonge supu: 2 💊
- Pilipili nyekundu paprika: kiasi 🌶️
- Bizari zote saga: 2 vijiko vya supu 🌿
- Viazi: 4 🥔
- Mafuta: 2 mug 🛢️
- Samli: ½ kikombe 🧈
- Vitungu: 6 🧅
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
- Kwenye sufuria, tia nyama, saga nyanya na thomu, pilipili mbichi, na tangawizi.
- Mimina kwenye nyama na mtindi, tia nyanya kopo, bizari paprika, vidonge vya supu, chumvi, kisha changanya vyote pamoja na weka motoni.
- Katika sufuria nyingine, tia mafuta na samli, kaanga vitungu mpaka viwe rangi ya hudhurungi, kisha toa na weka pembeni.
- Kanga viazi na weka pembeni.
- Chukua mafuta kidogo uliyokangia, tia kwenye nyama, acha kwenye moto wa kiasi mpaka nyama iwive na maji ya punguke.
- Tia viazi na vitunguu vivunje-vunje, tia ndani ya nyama, acha moto mdogo.
Vipimo Vya Wali 🍚
- Mchele - 5 mug 🍚
- Maji - kiasi 💧
- Chumvi - kiasi 🧂
- Mafuta uliyokaanga vitungu - kiasi 🧅
- Rangi ya biriani - ¼ kijiko cha chai 🟠
- Zafarani - ½ kijiko cha chai
Namna Ya Kutarisha Na Kupika Wali
- Osheni mchele na uroweke kwa saa. 🧼🍚
- Chemsha maji, kama magi 10 hivi, na chumvi. 🧂💧
- Tia mchele kwenye maji na uache uchemke mpaka kiini kiive nusu. 🕒
- Mwaga maji na chuja. 🍚💧
- Mimina mchele juu ya nyama, tia rangi na mafuta kwa juu, kisha funika. 🍗🟠
- Acha kidogo kwenye oveni kwa dakika 20 hivi, kisha epua ikiwa tayari. 🔥⏲️
- Pata kiungo
- X
- Barua pepe
- Programu Nyingine
Maoni