🥩🥗🍛BIRIANI YA NYAMA YA NG'OMBE

 NAMNA YA KUPIKA BIRIANI YA NYAMA YA NG'OMBE



VIPIMO VYA MASALA

  • Nyama vipande: 3 LB 🥩
  • Mtindi: ½ kopo 🥄
  • Kitunguu (thomu/galic): 1½ kijiko cha supu 🧄
  • Tangawizi: 1½ kijiko cha supu 🌿
  • Nyanya: 2 🍅
  • Pilipili mbichi: kiasi 🌶️
  • Nyanya kopo: 4 vijiko vya supu 🍅
  • Vidonge supu: 2 💊
  • Pilipili nyekundu paprika: kiasi 🌶️
  • Bizari zote saga: 2 vijiko vya supu 🌿
  • Viazi: 4 🥔
  • Mafuta: 2 mug 🛢️
  • Samli: ½ kikombe 🧈
  • Vitungu: 6 🧅

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

  1. Kwenye sufuria, tia nyama, saga nyanya na thomu, pilipili mbichi, na tangawizi.
  2. Mimina kwenye nyama na mtindi, tia nyanya kopo, bizari paprika, vidonge vya supu, chumvi, kisha changanya vyote pamoja na weka motoni.
  3. Katika sufuria nyingine, tia mafuta na samli, kaanga vitungu mpaka viwe rangi ya hudhurungi, kisha toa na weka pembeni.
  4. Kanga viazi na weka pembeni.
  5. Chukua mafuta kidogo uliyokangia, tia kwenye nyama, acha kwenye moto wa kiasi mpaka nyama iwive na maji ya punguke.
  6. Tia viazi na vitunguu vivunje-vunje, tia ndani ya nyama, acha moto mdogo.

Vipimo Vya Wali 🍚

  • Mchele - 5 mug 🍚
  • Maji - kiasi 💧
  • Chumvi - kiasi 🧂
  • Mafuta uliyokaanga vitungu - kiasi 🧅
  • Rangi ya biriani - ¼ kijiko cha chai 🟠
  • Zafarani - ½ kijiko cha chai 

Namna Ya Kutarisha Na Kupika Wali

  1. Osheni mchele na uroweke kwa saa. 🧼🍚
  2. Chemsha maji, kama magi 10 hivi, na chumvi. 🧂💧
  3. Tia mchele kwenye maji na uache uchemke mpaka kiini kiive nusu. 🕒
  4. Mwaga maji na chuja. 🍚💧
  5. Mimina mchele juu ya nyama, tia rangi na mafuta kwa juu, kisha funika. 🍗🟠
  6. Acha kidogo kwenye oveni kwa dakika 20 hivi, kisha epua ikiwa tayari. 🔥⏲️


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

JINSI YA KUPIKA MIKATE YA CHILA (VIBIBI)

🌿🥩🍌NDIZI ZA NYAMA

VILEJA VYA JICHO LA NGAMIA

🍗🥘🍲PILAU YA KUKU

JINSI YA KUPIKA NJEGERE ZA NAZI 🍲

🍪🍯VILEJA VYA CARAMEL

JINSI YA KUPIKA VITUMBUA

🌼🌺VILEJA VYA JAM