JINSI YA KUPIKA BIRIANI YA KUKU WA KUCHOMA (GRILLED CHICKEN BIRIANI)
MAHITAJI NA VIPIMO
π Mchele wa Basmati/Pishori - 4 vikombe
π Kuku
π§
Vitunguu - 3
π
Nyanya/Tungule - 2
π« Tangawizi mbichi ilosagwa - 2 vijiko vya supu
π§ Kitunguu saumu (thomu/galic) kilosagwa - 1 kijiko cha supu
πΆ️ Pilipili mbichi nzima - 3
π Ndimu - 2
π Garama Masala/bizari mchanganyiko - 1 kijiko cha supu
πΏ Haldi/tumeric/bizari manjano - 1 kijiko cha chai
πΆ️ Pilipili ya unga nyekundu - 1 kijiko cha chai
π₯ Mtindi/Yoghurt - 3 vijiko vya supu
π’️ Mafuta - ½ kikombe
HATUA ZA UPISHI
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
- π Osha mchele, kisha roweka.
- π§Ό Safisha kuku vizuri, mkate vipande vya saizi ya kiasi na uweke katika bakuli.
- π₯£ Katika kibakuli kidogo, changanya:
- π« Tangawizi mbichi
- π§ Thomu
- π Bizari zote
- πΆ️ Pilipili nyekundu ya unga
- π§ Chumvi
- π₯ Mtindi
- π Ndimu (kamua).
- π₯ Punguza mchanganyiko kidogo weka kando.
- Mchanganyiko uliobakia, tia katika bakuli la kuku na uchanganye vizuri ili kuku arowanike (marinate) kwa dakika chache, hata nusu saa au zaidi.
- π Weka kuku katika treya ya kuoka au kuchoma katika oveni, kisha mchome (grill) huku ukiwa unageuzageuza hadi aive. Epua na weka kando.
- π§ Katakata vitunguu, π nyanya/tungule, na πΆ️ pilipili boga, kisha weka kando.
- π’️ Katika sufuria ya kupikia biriani, tia mafuta na kaanga vitunguu hadi vigeuke rangi ya hudhurungi (brown).
- Tia nyanya, pilipili mbichi, pilipili boga, na mchanganyiko uliopunguza awali.
- π₯ Tia kuku na uchanganye vizuri.
- ⏳ Wakati unakaanga vitunguu ili kuokoa muda, huku chemsha mchele hadi uive nusu kiini, mwaga maji na chuja.
- π₯ Punguza masala nusu yake na uweke kando.
- π Mimina wali kiasi juu ya masala, kisha mimina masala yaliyobakia, na juu yake tena mimina wali.
- π₯ Funika na upike katika oveni hadi uive.
- π½️ Changanya unapopakua katika sahani.
Biriani yako iko tayari! π

Maoni